Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Biashara ya utumaji pesa kupitia mitandao si mali ya serikali-UNCTAD

Mukhisa Kituyi (kushoto) katibu Mkuu wa UNCTAD akiwa na Isabelle Durant (kulia) naibu Katibu Mkuu wa UNCTAD katika wiki ya ecommerce 2018.
Picha na UN/Jean-Marc Ferré
Mukhisa Kituyi (kushoto) katibu Mkuu wa UNCTAD akiwa na Isabelle Durant (kulia) naibu Katibu Mkuu wa UNCTAD katika wiki ya ecommerce 2018.

Biashara ya utumaji pesa kupitia mitandao si mali ya serikali-UNCTAD

Ukuaji wa Kiuchumi

Huduma ya mfumo wa kupokea  pesa  kutoka ughaibuni kupitia teknolojia ya mitandao na apu mbalimbali inazidi kushika kasi barani Afrika  na katika mataifa mengine yanayoinukia imesema kamati ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo na biashara UNCTAD.

Kwa mujibu wa  UNCTAD huduma hiyo imesaidia sana mamilioni ya watu wa masikini ambao hupokea fedha kutoka kwa jamaa zao walioko ughaibuni. Hata hivyo huduma hiyo inaanza kukukabiliwa na changamoto kufuatia baadhi ya serikali kuweka kodi kubwa katika biashara hiyo,jambo ambalo limezusha mjadala mkali.

Dkt Mukhisa Kituyi, ni Katibu Mkuu wa  UNCTAD,akiwa kwenye mkutano wa maendeleo endelevu mjini New York Marekani  alizungumzia suala hilo.

(SAUTI YA MUKHISA KITU)

Na kuhusu mipango ya mataifa ya Afrika kuwa na sarafu moja amesema

(SAUTI YA MUKHISA KITUI )