Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi wenye matatizo ya figo Jordan nyota ya jaha yawaangazia

Zaidi ya wakimbizi 14,500 wa Syria sasa wamehifadhiwa katika kambi ya Za'atri Jordan. Picha:UNHCR/A.McDonnell

Wakimbizi wenye matatizo ya figo Jordan nyota ya jaha yawaangazia

Afya

Wakimbizi wa Syria takriban 171 wanaoishi nchini Jordan wamekuwa wanasumbuliwa na matatizo ya figo na tiba yake ni gharama kubwa wasiyoweza kuimudu hadi sasa  ambapo habari njema imewaletea matumaini mapya. 

Wakimbizi hao ambao wengi ni masikini na hata mlo wao ni lazima wapewe msaada , walianza kupoteza matumaini kwani kama hawawezi kumudu kununua chakula watawezaje kumutu tiba ya dola 11,000 

Ndipo mfuko wa usaidizi wa kibinadamu wa Jordan (JHF) ukaingilia kati kunusuru maisha yao. Baada ya kuanza kupoteza matumaini ikizingatiwa kwamba watu hao ni wakimbizi  hivi sasa wanapata matibabu ya bure kwa hisani ya mfuko huo.

Miongoni mwao   ni Fayzeh Faeq Zardan, huku machozi yakimlengalenga anasema peremende tu ya mwanangu ni mtihani sembuse dawa “nimemwambia mtoto wangu wa kiume wa miaka mitatu kwamba HAPANA kwamba  hatapata peremende …hatuwezi kumudu kuzinunua.”

Image
Kambi ya Zaatari, Jordan. Picha:UNHCR/J. Kohler /September 2013


Vita vinavyoendelea Syria kwa mwaka w asaba sasa vimewafanya watu zaidi ya laki sita kukimbilia Jordan tangu 2014 na asilimia kubwa wanapatiwa msaada namfuko huo wa usaidizi wa Jordan.


Zardan  mwenye umri wa miaka 38 ni mkimbizi kutoka  mji wa magharibi mwa Syria wa Homs naye ni mgonjwa wa figo.“Sina hata pesa za kulisha familia yangu au za kugharimia sindano hii,’ amesema huku akionyesha mashine ilioko kwenye mkono wake.


Mashine hiyo humsaidia mgonjwa wa figo kutoa uchafu pamoja na chumvi ya ziada mwilini na majimaji kutoka kwenye   damu ilikuwezesha figo kufanya kazi.


Mbali na mashine hiyo pia kwa kipindi cha miaka mitatu amekuwa akipata sindano za kila wiki kutoka katika zahanati ya chama cha mwezi mwekundu cha Jordan.


Mita chache kutoka kitanda chake   ni mgonjwa mwingine Ghassan Nader Al Barq mwenye umri wa miaka 51. Alianza shida ya figo akiwa Syria miaka minane iliyopita , na alikimbilia Jordan miaka sita iliyopita na akapata tiba ndogo katika  hospital ya binafsi mjini Amman lakini gharama zilikuwa juu akashindwa kumudu.

Image
Mama na mwanawe kutoka Syria katika kambi ya Zaátri nchini Jordan (Picha© UNHCR/S.Malkawi)


Kati ya  wakimbizi hao 171 kutoka Syria walio na matatizo ya figo 124 kati yao wanapata matibabu kupitia  mfuko wa JHF, ilhali 37 wanatibiwa kupitia msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi, UNHCR, na 10 kupitia asasi mbalimbali za kiraia.


Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2016 ya wizara ya afya ya Jordan, gharama ya kutibu figo ni kwa wastani wa dola  11,000 kwa kila mgonjwa na asilimia 93 ya wakimbizi  walioko Jordan hawawezi kumudu.