Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Poland hakikisheni magereza yanatumiwa vyema UN

UN Photo/Martine Perret
Moja wa kizuizi
UN Photo/Martine Perret

Poland hakikisheni magereza yanatumiwa vyema UN

Sheria na Kuzuia Uhalifu

Poland imesonga mbele katika kuimarisha mazingira ya maeneo ya kuweka vizuizini watuhumiwa nchini humo lakini hatua zaidi zinapaswa kuchukuliwa ili kuimarisha zaidi, ikiwemo hatua za ulinzi na kuepusha matumizi holela ya kutumia vizuizi hivyo.

Ushauri huo  umetolewa leo mjini Warsaw Poland  na wajumbe wa kamati ndogo ya Umoja wa Mataifa ya kuzuia mateso wakati wakiwasilisha mbele ya mamlaka za nchi hiyo ripoti yao ya awali ya siri kuhusu jinsi ya kuimarisha ulinzi wa watu walionyimwa uhuru wao kutokana na mateso, ukatili na vitendo visivyo ya kibinadamu.

Kiongozi wa ujumbe huo Bi Aisha  Shujune Mohammad amesema ingawa wanapongezahatua za Poland lakini bado ichukue hatua zaidi kwenye haki za  msingi za ulinzi.

Pia wamesema wanaamini kwamba matumizi ya mbadala wa kizuizi yatapunguza idadi ya watu walioko korokoroni na hivyo kuboresha mazingira ya maeneo hayo.

Seli moja katika magereza Magere
UNICEF/Rajat Madhok
Seli moja katika magereza Magere

 

Ujumbe huo ulitembelea sehemu mbalimbali kunakozuliwa watu na kupata kwa undani   jinsi  mfumo wa vituo vya magereza ulivyo kwa sasa.

Kamati hiyo huwa inachunguza  jinsi mataifa yaliyoridhia  itifaki ya mkutano dhidi ya utesaji-OPCAT yanavyotekeleza majukumu yao ya mkataba huo pamoja na  kuunda mfumo huru wa kitaifa kuhusu uzuaji.

Poland illiridhia itifaki hiyo mwaka 2005.