Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sitisheni mapigano Syria ili misaada ifikie wahitaji- Grandi.

Familia ambazo zimepoteza makazi kutoka Quneira, kusini magharibi mwa Syria karibu na Golan. Familia zinatafuta mahali pa kukaa hazina.
UNICEF/Alaa Al-Faqir
Familia ambazo zimepoteza makazi kutoka Quneira, kusini magharibi mwa Syria karibu na Golan. Familia zinatafuta mahali pa kukaa hazina.

Sitisheni mapigano Syria ili misaada ifikie wahitaji- Grandi.

Amani na Usalama

Nina wasiwasi na mapigano Kusini Magharibi mwa Syria ambapo raia wa kawaida ndio wamenaswa katika mapigano hayo.

Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, Filippo Grandi amesema hayo leo kupitia taarifa iliyiotolewa mjini Geneva Uswisi.

Mapigano hayo yanahusisha mashambulio ya anga na makombora mazito ambapo watu takriban watu 750,000 wako hatarini huku wengine 320,000 hawana makazi wakiishi kwenye mazingira magumu.

Kati yao yao 60,000 wamepiga kambi huko Nasib/Jaber ambacho ni kituo cha kuvuka mpaka kuingia Jordan.

  “Ingawa jamii za Syria  zimewakaribisha  watu hao waliopoteza makazi yao, bado  wengiwanalazimika kulala   nje ama wengine katika vibanda vya muda tu ambavyo si salama. Miongoni mwao ni watoto, wanawake, wazee, majeruhi na wagonjwa,” amesema Bwana Grandi.

 

Famila kutoka Quneira vijijini, kusini mashariki mwa Syria wakitatafuta mahala pa kukaa.
UNICEF/Alaa Al-Faqir
Famila kutoka Quneira vijijini, kusini mashariki mwa Syria wakitatafuta mahala pa kukaa.

Ameongeza kuwa miongoni mwa waliopoteza makazi ni wafanyakazi wa kutoa misaada ambao walijitolea kwa dhati kusaidia raia wakati wa mgogoro.

Kamishna Mkuu huyo wa wakimbizi amesema kuwa kipaumbele sasa ni kutafuta suluhisho la kisiasa ili kuweza kuwaondolea mateso zaidi watu wa Syria.

Wakati huo huo, Umoja wa Mataifa na washirika wake wanajaribu kadri ya uwezo wao  kutoa msaada muhimu kwa wakazi wa kusini-magharibi mwa Syria na pia katika upande mwingine Jordan.

Hata hivyo hali ya kiusalama inadumaza juhudi za kuwafikia watu hao.

Bw Grandi ameziomba pande zote kuzidisha juhudi za  kukomesha makabiliano, waruhusu misaada muhimu ifikishwe kwa walengwa na pia wakubali watoa misaada ya kibinadamu kufanya kazi yao ya kuhamisha majeruhi na pia kuwapatia wahitaji makazi ya muda.

Ameongeza kuwa ulinzi na usalama  wa raia  na watoa msaada ni muhimu mno.