Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kulemaa viungo sio kulemaa akili- Dkt. Sankok

Adeline Hatangimana (kushoto)  mwenye umri wa miaka 30 ambaye alipoteza jicho ,
UNHCR/Colin Delfosse
Adeline Hatangimana (kushoto) mwenye umri wa miaka 30 ambaye alipoteza jicho ,

Kulemaa viungo sio kulemaa akili- Dkt. Sankok

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Kuwa na ulemavu wa aina yoyote ile hakumaanishi umelemaa akili na watu wenye ulemavu wana uwezo mkubwa na mchango katika jamii kama walivyo watu wengine wasio na ulemavu amesema Dkt. kutoka jamii ya Wamasai ya Narok nchini Kenya

Huyu ni Dr Helen Sankok mtaalamu wa masuala ya afya na uzazi wa mpango katika jamii ya Wamaasai huko Narok nchini Kenya, ambaye kwa zaidi ya muongo  na nusu sasa anaishi na mumewe mwenye ulemavu wa miguu pamoja na watoto wao.

Anasema katika jamii yake bado ni changamoto kubwa kuwakubali watu na hata watoto wanaozaliwa na ulemavu hususan vijijini.

Mtihani huo haukumsamehe Dr.  Sanko hasa pale alipoijulisha familia yake anataka kuolewa na mtu mwenye ulemavu wa miguu.

Hata hivyo baada ya jitihada kubwa za serikali, wanaharakati na makundi ya watu wenye ulemavu kuielimisha jamii anasema nuru imeanza kuangaza gizani kuanzia kwa familia yake