Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Zeid aikumbusha Iran, hata akikosa nini mtoto haistahili kunyongwa

Kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa , Zeid Ra'ad Al Hussein
Picha ya UN/Jean-Marc Ferré
Kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa , Zeid Ra'ad Al Hussein

Zeid aikumbusha Iran, hata akikosa nini mtoto haistahili kunyongwa

Haki za binadamu

Vitendo vya unyongaji wa watoto wahalifu vinavyotekelezwa nchini Iran ni kinyume na wajibu wa nchi hiyo kama mwanachama wa  mkataba wa  haki za watoto na sheria za kimataifa kuhusu haki za kisiasa na kijamii.

Hayo yamesemwa leo mjini Geneva Uswisi  na Kamishna wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, Zeid Ra’ad Al Hussein kufuatia Iran kutekeleza hukumu ya kifo dhidi ya kijana Aboklfazi Chezani Sharahi, kwa kosa la kumuua mtu mmoja kwa kumdunga kisu.

Sharahi alikuwa na umri wa miaka 15 tu alipohukumiwa kifo na mahakama moja ya nchini humo, na alinyongwa jana Jumatano.

Zeid Al Hussein amelaani hatua hiyo, akisisitiza kuwa kuwanyonga watoto wahalifu ni ukiukaji wa  sheria za kimataifa  na mtoto hapaswi kunyongwa hata kama amefanya kosa gani.

Sharahi ni  mtoto wa nne kunyongwa nchini Iran tangu tangu kuanza kwa mwaka huuhuku watoto wengine watano walinyongwa mwaka jana.

Zeid amesema kuna taarifa za watoto wengine 85 wanaosubiri kunyongwa na kuongeza ,  “tunaelewa  kuna mtoto mwingine Mohammad Kalhori, hukumu yake ya kunyongwa itatekelezwa wakati wowote lakini naiomba serikali ya Iran kutotekeleza hukumu hiyo na badala yake kuigeuza adhabu ya kifo kuwa kifungo cha maisha.”

Pia kamishna  ameelezea wasiwasi wake  wa kutokuwepo na uwazi kabla ya kutekeleza hukumu ya kifo nchini Iran akisema kwa kutotoa taarifa za wakati wa kutekeleza hukumu hiyo hakuweki rehani tu roho ya mfungwa bali pia kunawaweka roho juu familia na jamaa zake hali inayosababisha msongo wa mawazo.

Zeid amesema ofisi yake iko tayari kuisaidia serikali ya Iran kufuata  wajibu wake kuelekea haki za binadamu na sharia za kimataifa kuhusu haki za watoto waliofanya