Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nimepokea kwa hofu taarifa za mlipuko wa bomu Ethiopia:Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akihutubia kikao cha Muungano wa Afrika mjini Adddis Ababa wakati fulani
Picha ya UN /Antonio Fiorente
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akihutubia kikao cha Muungano wa Afrika mjini Adddis Ababa wakati fulani

Nimepokea kwa hofu taarifa za mlipuko wa bomu Ethiopia:Guterres

Amani na Usalama

Mtu mmoja ameripotiwa kufariki na wengine kadhaa kujeruhiwa  katika mlipuko uliotokea kwenye mkutano wa hadhara wa waziri mkuu mpya wa Ethiopia Abiy Ahmed siku ya Jumamosi.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ,amelaani vikali tukio hilo  la ghasia na kusema amepokea kwa hofu kubwa tarifa hizo za kusikitisha.

Image
Bendera ya Ethiopia. Picha: UM/Loey Felipe

 

Kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Katibu Mkuu“ametuma salamu za  rambirambi zake kwa jamaa za marehremu na kuwatakaia ahuweni ya haraka majeruhi wotena kuonyesha mshimanao wake na watu na serikali ya Ethiopia .