Nimepokea kwa hofu taarifa za mlipuko wa bomu Ethiopia:Guterres
Amani na Usalama
Mtu mmoja ameripotiwa kufariki na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mlipuko uliotokea kwenye mkutano wa hadhara wa waziri mkuu mpya wa Ethiopia Abiy Ahmed siku ya Jumamosi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ,amelaani vikali tukio hilo la ghasia na kusema amepokea kwa hofu kubwa tarifa hizo za kusikitisha.
Kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Katibu Mkuu“ametuma salamu za rambirambi zake kwa jamaa za marehremu na kuwatakaia ahuweni ya haraka majeruhi wotena kuonyesha mshimanao wake na watu na serikali ya Ethiopia .