Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi Nyarugusu msitoke kambini bila vibali- Kamishna Makakala

Baba na wanae katika kambi ya wakimbizi ya Nyargusu nchini Tanzania.(Picha:UM/Tala Loubieh)

Wakimbizi Nyarugusu msitoke kambini bila vibali- Kamishna Makakala

Wahamiaji na Wakimbizi

Wakimbizi wanaoishi kwenye kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma nchini Tanzania wametakiwa kuzingatia kanuni za kuwepo kwenye eneo hilo ili kuepuka mkono wa sheria.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini Tanzania Anna Peter Makakala amesema hayo alipozuru kambi hiyo inayohifadhi wakimbizi ambao idadi kubwa ni kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na Burundi.

(Sauti ya Anna Peter Makakala)

Takwimu za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR zinaonyesha kuwa kambi hiyo ina zaidi ya wakimbizi 134,000.