Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nchi masikini zapata mkombozi, Benki ya teknolojia:UN

Naibu Katibu Mkuu wa Umojawa Mataifa, Amina Mohammed(kulia) na Faruk Özlü (katikati) waziri wa sayansi, viwanda na Teknolojia
UNOHRLLS
Naibu Katibu Mkuu wa Umojawa Mataifa, Amina Mohammed(kulia) na Faruk Özlü (katikati) waziri wa sayansi, viwanda na Teknolojia

Nchi masikini zapata mkombozi, Benki ya teknolojia:UN

Masuala ya UM

 Chombo kipya chenye lengo la kushughulikia  changamoto  za mataifa maskini duniani kimezinduliwa rasmi hi leo mjini Gebze nchini Uturuki.

Chombo hicho ambacho ni  “Benki ya Teknolojia”, kitashughulikia matatizo ya nchi hizo maskini kupitia  sayansi, teknolojia pamoja na ubunifu.

Akihutubia wakati wa  uzinduzi  wa chombo hicho ,Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bi Amina Mohammed, amesema  uzinduzi huo ni wa muhimu katika kusaidia  mataifa yaliyo na maendeleo duni -LDCs kuweza kujiendeleza kwa kutumia faida za sayansi, teknolojia na ubunifu. Akisisitiza umuhimu wa chombo hicho wakati wa mkutano na waandishi wa habari mjini New York hii leo, kwa kumnukuu Bi Mohammed, msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric amesema

 (SAUTI YA STEPHANE DUJARRIC)

“Kuundwa kwa benki ya teknolijia kunadhihirisha azma ya ulimwengu kuhakikisha kwamba mataifa yote  yanaweza kutumia vifaa vya hali ya juu ili kufanikisha malengo yote endelevu

Baraza kuu la Umoja wa Mataifa, lilipitisha kuundwa kwa Benki ya Teknolojia , ili ibebe jukumu la kuimarisha uwezo wa maarifa au ufahamu wa mataifa 47 yenye maendeleo duni, kwa minajili  kuchochea maendeleo na ubunifu wa mifumo yake ya teknolojia ya kitaifa na kikanda ili kuweza kuvutia teknolojia ya nje kwa lengo la    kukuza uwezo wake wa ndani wa utafiti  na ubunifu.

Bi Mohammed amesema uzinduzi wa leo ni  tukio muhimu la kihistoria katika kusaidia mataifa yenye maendeleo duni kutumia faida za sayansi, teknolojia na ubunifu, ili kutilia  mkazo ufikiaji wa ajenda ya maendeleo yam waka 2030 ambayo inataka kuhakikisha  “hakuna atakaeachwa nyuma” kwani huo ndio ufunguo.

Ameongeza kuwa chombo hiki kinatarajiwa  kuboresha  matumizi ya kisayansi kwa mataifa maskini kuweza kupata uchumi ambao unaegemea maarifa.