Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Je wanavijiji watamudu nishati mbadala ili kulinda misitu Tanzania?

Kilimo, misitu na shughuli nyingine za matumizi ya ardhi hutoa tani zaidi ya bilioni 10 za gesi chafuzi. Picha: FAO / Daniel Hayduk

Je wanavijiji watamudu nishati mbadala ili kulinda misitu Tanzania?

Tabianchi na mazingira

Katika jitihada za pamoja za Umoja wa Mataifa  na serikali duniani kuhakikisha misitu inalindwa ili kudhibiti mabadiliko ya tabianchi, Tanzania imejiwekea mkakati kabambe wa  miaka 5 kwenda sanjari na lengo hilo.

Hayo yameelezwa na Dk Ezekiel Mwakaluka ambaye ni mkurugenzi wa Misitu na nyuki katika wizara ya maliasili na utalii nchini tanzania alipohojiwa na idhaa ya Umoja wa Mataifa jijini New York.

Akizungumzia changamoto ya uhifadhi wa misitu hususani kwa wananchi wa vijijini walio na kipato cha chini ambao kwa asimilia kubwa wanalazimika kutumia mkaa Dk Ezekiel alisema....

Na endapo serikali ina mpango wa kueneza umeme kuepusha hilo,  wanavijiji wanawezeshwa vipi kumudu gharama za umeme, wakati mkaa  na kuni wanapata bure ?