Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Badala ya beseni la chakula, watoto DRC wabeba beseni la mchanga

Watoto katika kambi mjini Kalemie mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya  Congo. Watoto kama huyo wanatumiwa kubeba mchanga ili kusaidia familia zao
Picha na UNICEF/Vockel
Watoto katika kambi mjini Kalemie mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Watoto kama huyo wanatumiwa kubeba mchanga ili kusaidia familia zao

Badala ya beseni la chakula, watoto DRC wabeba beseni la mchanga

Amani na Usalama

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, vita na janga la kibinadamu nchini humo vimesababisha watoto kulazimika kufanya kazi ili waweze kutunza familia zao. Grace Kaneiya na ripoti kamili.

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, vita na janga la kibinadamu nchini humo vimesababisha watoto kulazimika kufanya kazi ili waweze kutunza familia zao. Grace Kaneiya na ripoti kamili.

Ni msururu wa watoto wakiwa wamebeba magunia, makarai na magudulia yaliyojaa  mchanga wakitoka  fukwe za ziwa Tanganyika eneo la Kalemie, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC

Watoto hawa ni miongoni mwa mamia kwa maelfu ya watu ,wazee kwa watoto na wake kwa waume wanaohangaishwa   na migogoro inayokumba jimbo la Tanganyika lililo mashariki mwa nchi hiyo.

Umaskini, njaa na magonjwa vinawakabili licha ya kamisaada kama vile kutoka shirika la kuwahudumia wakimbizi-UNHCR bado watoto hawa wanaendelea kupambana ili waweze kuishi.

Mmoja wao ni Françoise Asani Philippe.

Watoto hawa wa kike na wa kiume baadhi yao wakiwa na umri wa miaka  mitano,  badala ya kubeba beseni au sahani za vyakula, wanabeba mabeseni ya mchanga ili apate kipato. Na hufanya kazi hii tangu saa kumi na nusu alfajiri.

Mchanga huu sana sana hutumiwa kujengea nyumba na malipo kwa watoto ni gharama ndogo. Mtoto hupewa sentí 30 ya dola kwa kila kilo 25 za mchanga anazobeba.

Hapa wazazi hawana la kufanya ila kuwaacha watoto wafanye kazi kama asemavyo baba mzazi wa Francoise, aitwaye Philippe Kika Malisawa.

“ Wazazi wetu hawakutufanyisha kazi  kiasi hiki. Tulikuwa tunakaa tu na baba zetu  wanatuletea chakula. Lakini sasa kwa sababu hatuna pa kuishi tunateseka tu.”