Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Viongozi wa Sudan Kusini wekeni maslahi ya watu wenu mbele -UN

David Shearer, mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Sudan Kusini akutana na wakazi wa Akobo
Picha ya UNMISS/Amanda Voisard
David Shearer, mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Sudan Kusini akutana na wakazi wa Akobo

Viongozi wa Sudan Kusini wekeni maslahi ya watu wenu mbele -UN

Amani na Usalama

Mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini wa UNIMISS amewahimiza viongozi nchini humo kuweka  maslahi ya watu wao kwanza  na kutumia wakati huu ili wasikilizane waweze kuleta  amani ya kudumu.

Mkuu wa UNIMIIS,David Shearer, ameyasema hayo mjini Addis Ababa katika mkutano wa ngazi za juu wa  jukwa la kuongeza matumaini ambapo ameeleza madhila yanayowakuta watu aliowashuhudia  alipozuru jimbo la Unity nchini  Sudan Kusini hivi majuzi, ambako mapigano yanaendelea.

“Nimeona uharibifu. Nimeona ‘tukuls’ zilizochomwa. Nimesikia wanawake na wasichana ambao walibakwa,watu waliouawa, na wengine maelfu ambao waliojificha katika vinamasi wakitoroka kuuawa’’, amesema.

David Shearer, ambae pia ni mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, amesema kuwa watu aliozungumza nao walimuomba  kupeleka ujumbe mzito katika mazungumzo hayo.

“Kwa niaba ya watu hao, nawaombeni, nawasihi, na kuhitaji kutoka kwenu, mtafute njia ya kuelewana, mpatane  ili mpate amani na kuweza kusaidia  watu hao niliowakuta, waweze kuishi maisha mazuri.”

Jukwa hilo ni nafasi kwa pande zote husika kuja pamoja kuendeleza mazungumzo ya amani kuhusiana na mkataba wa kusitisha uhasama  waliosaini miezi mitano iliyopita mjini Addis Ababa

Yeye mwenyekiti wa baraza la mawaziri wa IGAD Dr, Workneh Gebeyehu, amesema kuwa baraza lake liko tayari kuchukulia hatua dhidi ya yeyote  atakaekwenda kinyume na mkataba wa Addis Ababa.IGAD  ni kundi  linalojumuisha  mataifa  nane ya Afrika  katika masuala ya kiuchumi.