Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vikwazo vya kiuchumi Syria ni kigingi kwa misaada ya kibindamu

Mtaalam huru wa haki za binadamu wa Umoja kuhusu vikwazo vya kimataifa Idriss Jazairy.
Picha ya UN /Eskinder Debebe
Mtaalam huru wa haki za binadamu wa Umoja kuhusu vikwazo vya kimataifa Idriss Jazairy.

Vikwazo vya kiuchumi Syria ni kigingi kwa misaada ya kibindamu

Haki za binadamu

Mtaalam huru wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa asema , vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Syria vinaathiri utoaji wa  misaada ya kibinadamu kwa maelfu ya wathitaji nchini humo.

Bw Idriss Jazairy, aliyemaliza ziara ya siku 4 nchini humo kwa mwaliko wa serikali ya Syria, amesema amebaini kuwa vikwazo jivyo dhidi ya serikai ya Syria kwa namna moaja au nyingine vimekuwakizingiti kikubwa  katika ukuajii wa uchumi wa nchini hiyo na pia katika ufikishaji wa misaada ya kibinadamu kwa walengwa.

Katika ripoti yake bwana Jazairy amesema haungi mkono mgogoro wa Syria au  vitendo vya kikatili vinavyofanywa na serikali ya Syria, ila kwa mtazamo wa kibinadamu ongezeko la vikwazo vya kiuchumi tangu mwaka 2010 vimechangia sana kuporomoka kwa  uchumi na kuaathiri soko la ajira Syria kwa kiwango kikubwa huku mfumuko wa bei ukiongezeka kila uchao na kusababisha theluthi moja ya waSyria kukosa chakula.

Pia amesema anaamini kwamba wadau wote wenye nafasi ya kutoa misaada ikiwemo chakula, huduma ya afya, maji na misaada mingine  ya kibinadamu wanayo nafasi ya  kujiunga kwa pamoja kuwezesha mahitaji ya kibinadamu kuwafikia  watu ambao ni wahitaji .

Mtalamu huyo atarajia kuwasilisha ripoti yake mbele ya Baraza la haki za binadamu mwezi septemba mwaka  huu.