Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tusichoke kuwekeza katka elimu ya watoto Syria: Cappelaere.

Watoto wakimbizi kutoka Syria katika kambi ya Kawergosk magharibi mwa Erbil wakijisomea nje ya hema yao.
UNICEF/Romenzi
Watoto wakimbizi kutoka Syria katika kambi ya Kawergosk magharibi mwa Erbil wakijisomea nje ya hema yao.

Tusichoke kuwekeza katka elimu ya watoto Syria: Cappelaere.

Msaada wa Kibinadamu

Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia  watoto duniani UNICEF, imebaini kuwa licha ya vita vya zaidi ya  miaka 7 nchini Syria, watoto milioni 4.9 wameendelea kupata elimu, japo katika mazingira magumu .

Geert Cappelaere. ambaye ni mkurugenzi wa UNICEF ukanda wa Mashariki  ya kati na kaskazini mwa Afrika amesema, misaada kutoka kwa  wahisani na kazi nzuri ya kujitolea inayofanywa na  waalimu nchini humo ndio sababu kuu ya kufikia mafanikio hayo ya elimu kwa watoto.

Aidha ripoti imesema zaidi ya asilimia 90 ya watoto ambao wanapata elimu katika shule za umma wapo Syria na wengine ni wakimbizi wa Syria  walioko Lebanon na Jordan ambao wanaendelea kupata elimu  katika shule za umma za nchi hizo.

Kwa mujibu wa UNICEF japo wamefanikiwa kwa kiasi, mgogoro wa Syria ambao umedumu kwa  zaidi ya miaka  saba umewakosesha elimu zaidi ya  watoto milioni 2.8, ambapo tangu mwaka 2011 shule  Zaidi ya 309 zimeharibiwa.

Ripoti imeongeza kuwa shule moja kati ya 3 zimesambaratishwa kabisa na kusababisha zaidi ya asilimia 40 ya watoto wenye umri kati ya miaka 15 na 17 kutokuwa shuleni  na kuishia kwenyemakundi ya kigaidi baada ya kurubuniwa na wahalifu.