Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watoa misaada ni lazima walindwe. Guterres

Shule iliyobomolewa vibaya katika mapigano mjini Taizz
UNICEF/UN026944/Basha
Shule iliyobomolewa vibaya katika mapigano mjini Taizz

Watoa misaada ni lazima walindwe. Guterres

Amani na Usalama

Mfanya kazi mmoja wa kutoa misaada  ya kibinadamu wa chama cha msalaba  mwekundu na hilali nyekundu-ICRC ameuawa na watu wasiojulikana waliokuwa wamebeba silaha  mjini Taizz nchini Yemen

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres , kupitia  taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Stephane Dujarric , amelaani shambulio hilo na kutaka waliotekeleza kitendo hicho wakamatwe na kuchukuliwa hatua za sheria.

Amekariri kuwa pande zote husika katika mgogoro nchini Yemen ni sharti wawape ulinzi watoa misada ya kibinadamu kwa watu wa Yemen zaidi ya milioni mbili wanaohitaji msaada.

Taarifa za tukio hilo zinasema kuwa mfanya kazi huyo aliuawa katika viunga vya Taizz, wakati genge la watu wenye silaha lilipovamia gari la chama cha msalaba mwekundu.