Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNFPA yajipanga kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake ifikapo 2030

Monica Ferro, mkurugenzi wa UNFPA Geneva akiwa  kwenye mkutano wa kikanda wa  WHO mjini Coimbra, Ureno
UN News
Monica Ferro, mkurugenzi wa UNFPA Geneva akiwa kwenye mkutano wa kikanda wa WHO mjini Coimbra, Ureno

UNFPA yajipanga kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake ifikapo 2030

Afya

Mkutano wa kikanda ulioandaliwa na shirika la afya ulimwenguni WHO huko Coimbra Ureno, umeyakutanisha mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa na ya kibinadamu ili kujadili mikakati madhubuti kuhusu upatikanaji wa bima ya afya hususan kwa watu wasio na uwezo katika nchi masikini duniani.

Bi Monica Ferro ni mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu    UNFPA katika ofisi ya Geneva Uswisi ambaye kwenye mahojiano na idhaa wa Umoja wa Mataifa amesema amewakilisha shirika lake kwenye mkutando huo ili kujadili umuhimu wa kuwekeza katika afya ya mwanamke  ikiwa ni njia ya kukabili matatizo ya kimaendeleo na ya kijamii .

Sauti ya Monica Ferro

Ni muhimu kuwekeza katika afya yao, ni muhimu kuwekeza katika upatikanaji wa uzazi wa mpango ili kuwapa fursa ya kupanga mwelekeo wa maisha ya  baadaye  katika kupata elimu ya kutosha  ili  kuwapa  uwezo na ujasiri wa kuamua maisha yao ya baadaye na pia fursa ya ajira nzuri kama ilivyo kwenye mpango wetu wa kutomuacha  mtu yeyote nyuma.

Na kuhusu mikakati itakayojadiliwa  kwenye mkutano huo ili  kufikia malengo ya  mendeleo endelevu ya mwaka  2030 Bi Ferro amesema

Sauti ya Monica Ferro

 Majadiliano yetu katika mkutano huu yanajikia katika vipengele vitatu ambavyo UNFPA imejiwekea  ili kufikia 2030.  Vipengele hivyo ni  kutosheleza huduma   ya afya ya uzazi , kusiwepo na vifo wakati wa kujifungua, na kusiwepo na vitendo vya aina yeyote vya ukatili dhidi ya wanawake ikiwa ni pamoja na  ukeketaji kwa  wasichana.