Kumuwezesha mwanawake ni kuwezesha maendeleo : Sofia Donald
“Wanawake wakijengewa uwezo kiuchumi wataweza kukabiliana na matatizo mbalimbali katika jamii inayowazunguuka ikiwemo suala la tabianchi na mazingira na pia ukatili wa kijinsia”
Hiyo ni kauli ya Sofia Donald mratibu wa shirika la sauti ya wanawake ukerewe nchini Tanzania.
Akizungumza na idhaa ya kiswahili ya Umoja wa Mataifa Bi Sofia amesema, changamoto nyingi zinazowakabili wanawake hususan wa vijjinii zinatokana na hali duni ya maisha, na iwapo watawezeshwa kupitia miradi mbalimbali ya kiuchumi ni dhahiri kwamba wanawake wanaweza kukabiliana na matatizo ya tabianchi na vile vile ukatili wa kingono vijijini.
(Sauti ya Sofia Donald)
Na kuhusu hatua zilizochukuliwa na shirika la sauti ya wanawake ukerewe kuhusu utekelezaji wa agenda ya Umoja wa Mataifa ya melengo ya maendeleo endelevu kwa wanawake Bi Sofia amesema…..
(Sauti ya Sofia Donald)