Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ujenzi mpya Iraq wapigwa jeki na WFP na Japan

Darasa moja katika jengo la shule lililobomolewa wakati wa vita huko Ninewa Governorate, Iraq
UNICEF/UNI199916/Jemelikova
Darasa moja katika jengo la shule lililobomolewa wakati wa vita huko Ninewa Governorate, Iraq

Ujenzi mpya Iraq wapigwa jeki na WFP na Japan

Amani na Usalama

Wakati serikali ya Iraq ikiibuka kutoka kwenye machafuko ya miaka minne, shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP ,limepokea dola milioni 10 kama mchango wa serikali ya Japan kusaidia ujenzi mpya Iraq.

Mchango huo utalisaidia shirika la WFP kuongeza shughuli za kuinua kipato na maisha ya Wairaq 9000 wasiojiweza. Na shughuli hizo zinalenga kufufua kilimo kupitia ukarabati wa mifereji ya mifumo wa umwagiliaji iliyoharibiwa kutokana na vita.

Fedha hizo pia zitatumia kutoa msaada wa chakula kwa muda wa miezi saba, kwa wakimbizi wa Syria 23,000 wanaoishi katika jimbo la Kurdistan nchini Iraq kupitia mpango wa vocha.

Image
Mwanamke mYazidi Kurd kutoka Sinjar aliyenaswa na wanamgambo wa ISISL,. Yuko kambi ya wakimbizi wa ndani ya Mamilyan nchini Iraq. Picha: Giles Clarke/ Getty Images Reportage

 

Kwa mujibu wa WFP mchango huo ni sehemu ya dola milioni 100 za fungu linalohitajika katika msaada wa kibinadamu kwa ajili ya wakimbizi wa ndani, watu wanaorejea makwao, wakimbizi walioenda nje na jamii zinazowahifadhi.

Tangu mwaka 2014 Japan imeshachangia dola milioni 60.3 kwa shughuli za usaidizi za WFP nchini Iraq.