Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN yalaani shambulio nchini Ufaransa.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres
Picha ya UN /Rick Bajornas
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres

UN yalaani shambulio nchini Ufaransa.

Amani na Usalama

Umoja wa Mataifa unasimama bega kwa bega na serikali ya ufaransa katika vita dhidi ya ugaidi pamoja na misimamo mikali ya imani.

Kauli hiyo imetolewa leo  na Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guteress, kupitia msemaji wake  Stéphane Dujarric kufuatia shambulio la kigaidi dhidi ya Ufaransa siku ya Ijumaa.

Katibu mkuu amevipongeza vikosi vya usalama vya Ufaransa kwa hatua ya haraka ambayo ilisaidia kuokoa maisha ya raia na pia kutoa pole kwa familia za wale walioathirika tukio hilo na wananchi na serikali ya Ufaransa.

Pia Katibu Mkuu amewatakia wale waliojeruhiwa wapate nafuu haraka.

Shambulio hilo la kigaidi lilitokea  katika mji wa Trebes ulioko kusini magharibi mwa Ufaransa.