Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Rais wa Baraza kuu Miroslav ahitimisha ziara yake Colombia

Rais wa Baraza Kuu Miroslav Lajčák akihutubia mkutano wa baraza kuu kuhusu vipaumbele vyake kwa mwaka 2018. Picha na: UN/Manuel Elias

Rais wa Baraza kuu Miroslav ahitimisha ziara yake Colombia

Masuala ya UM

Rais wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa, Bwana Miroslav Lajčák, amehitimisha  ziara  yake ya siku mbili  nchini Colombia ambako alikutana na vyongozi wa ngazi ya juu serikalini na  asasi za kiraia ili  kuzungumzia azma ya utekelezaji wa amani na maendeleo andelevu SDGs.

 

Katika ziara yake Bw. Lajčák  alikutana na rais wa Colombia Bw. Juan Manuel Santos Calderón ambapo wawili hao alizungumzia mchakato wa  amani na ulinzi, ushirikiano baina  ya Colombia na Umoja wa Mataifa, maendeleo ya kiuchumi kikanda, uhamiaji na  malengo ya maendeleo   endelevu ya kudumu (SDGs).


Aidha, Bw. Lajčák alimshukuru rais Santos kwa kukubali kuhudhuria mkutano wa ngazi ya  juu kuhusu uimarishaji wa  amani ya kudumu  Colombia uliofanyika jijini Newyork  mnamo tarehe 24 na 25 Aprili mwaka jana., na pia  kwa ushirikiano wake na mkurugenzi wa mipango ya taifa Luis Fernando Mejía katika uzinduzi wa mkakati wa kitaifa Colombia wa kutekeleza SDGs.

Bwana Martín Santiago Herrero ambaye ni mwakilishi wa huduma za kibinadamu za Umoja wa Mataifa nchini Colombia amesema, ziara ya rais wa Baraza kuu nchini humo ni ishara ya ushirikiano baina Umoja wa Mataifa na Colombia katika uimarishaji na utekelezaji wa amani na maendeleo endelevu endelevu .