Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tusaidie serikali kumkomboa mwanamke- Dkt. Soko

Dtk.Grace Soko, Mkurugenzi mtendaji wa YWCA Tanzania akiwa kwenye mkutano wa kamisheni ya hali ya wanawake CSW62 jijini New York
UNnewskiswahili/Patrick Newman
Dtk.Grace Soko, Mkurugenzi mtendaji wa YWCA Tanzania akiwa kwenye mkutano wa kamisheni ya hali ya wanawake CSW62 jijini New York

Tusaidie serikali kumkomboa mwanamke- Dkt. Soko

Wanawake

Wakati mkutano wa kamisheni ya hali ya wanawake CSW62 ukiendelea jijini New York, Marekani  wawakilishi wa mashirika ya kiraia kutoka Tanzania wamezungumziaumuhimu wa  suala la uwezeshaji  wanawake vijijini kupitia mafunzo mbalimbali waliyoyapata kwenye mkutano huu.

Mmoja wa wawakilishi hao ni Grace Soko Mkurugenzi Mtendaji chama cha wanawake wakristo Tanzania, YWCA, ambaye akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amesema kwa kuhudhuria CSW, amepata nafasi ya kubadilishana mawazo na mataifa mengine na pia kupata taswira ya dunia nzima kuhusu masuala ya wanawake,  na kwamba….
(Sauti y a Dkt. Grace Soko)

Halikadhalika amesema YWCA katika ajenda zake, wamepatia kipaumbele suala la kupiga vita ukatili wa kingono dhidi ya wanawake nchini Tanzania ambapo wameongeza vituo vya usaidizi kwa wanawake   katika kanda ya ziwa ambako visa vya  ukatili dhidi ya wanawake vinazidi kuongezeka kila uchao.
(Sauti y a Dkt. Grace Soko)