Faida ya kuinuliwa nawe uinuwe wengingine:KPL
Kikao cha 62 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani kikiendelea kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani, washiriki wanaendelea kupigia chepuo juhudi za ukombozi wa wanawake na wasicha wa vijijini kwa kuelezea wanachokifanya. Leo tumekutana na mwanaharakati kutoka nchini Kenya.
Bi Khoboso Hargura Hadichareh ni miongoni mwa wanaharakati hao ni mwanzilishi wa mfuko wa kujitolea uitwao KPL, yaani Kargi Pastroralist Link kwa ajili ya kusaidia jamii ya wafugaji wa kuhamahama wa Rendile kwenye eneo la Marsabit jimbo la Kaskazini Mashariki .
Jamii hiyo inaghubikwa na changamoto lukuki zikiwemo, ukosefu wa maji safi na salama, ufahamu mdogo wa masuala ya ulemavu, masuala ya ukimwi na wanawake kukosa sauti, lakini kubwa zaidi ni tatizo la elimu hasa kwa mtoto wa kike na ndicho kilichomfanya Khoboso kuchukua hatua kwani
(SAUTI YA KHOBOSO ARGURA)
Na wito wake ndio huu
(SAUTI YA KHOBOSO HARGURA)
TAGS: CSW62, wanawake, rendile, elimu, KPL, Khoboso Hargura Adichareh