Zeid aikemea Ufilipino kumuorodheshwa mwanarakati wa haki kama gaidi
Kamishna mkuu wa haki za binadamu, Zeid Ra’ad Al Hussein amekemea hatua za utawala wa Ufilipino za kumuweka katika orodha ya magaidi, uwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu za watu asili, Victoria Tauli-Corpuz.
Bwana Zied amesema kitendo hicho hakikubaliki na ni lazima kijibiwe.
(Sauti ya Zeid Ra’ad Al Hussein)
“Bila shaka hii haiwezi kukubalika dhidi ya muwakilishi maalum akifanya kazi kwa niaba ya jamii ya kimaaifa kufanyiwa hivyo na ambaye ujuzi wake unahitajika mno na bazala la haki za binadamu.”
Akimnukuu mwakilishi mwenyewe akisem akuwa huenda hatua hiyo imechochewa na uamuzi wake wa kukaripia uawala dhidi ya mauaji ya kiholela kwa wanaodaiwa kuwa wanajihusisha na madawa ya kulevya, vita alivyoanza kiongozi wa sasa wa Ufilipino.
Victoria na wenzake wanalaumiwa kuwa wanachama wa chama cha Kikomunist cha CCP pamoja na New Peoples Army-NPA.
Pia hivi majuzi imeelezwa kuwa rais wa sasa wa Ufilipino alidaiwa kutumia maneno yasiyofaa kumuhusu Muwakilishi huyo wa Umoja wa Mataifa. Hilo nalo kamishna Zeid amelishutumu.
(Sauti ya Zeid Ra’ad Al Hussein)
“Matamshi kama haya kwa kweli hayakubaliki…hayakubaliki.
Ameongeza kuwa kiongozi huyo wa Ufilipino anafaa kuchunguzwa na wataaalamu wa masuala ya akili.