Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Licha ya vikwazo vya usalama kampeni ya chanjo lazima isonge mbele- WHO

Msichana Sudan Kusini akipokea chanjo ya kipindupindu.Picha:UN Picha / JC McIlwaine

Licha ya vikwazo vya usalama kampeni ya chanjo lazima isonge mbele- WHO

Msaada wa Kibinadamu

Shirika la Afya ulimwenguni WHO, limesema pamoja na kuwa linakabiliwa na tatizo la usalama bado linaendeleza kampeni ya chanjo Sudan kusini, hususani katika maeneo Jonglei na ukanda wa mto Nile ili kupunguza  kusambaa kwa magonjwa ya donda koo na mengine.

Bwana Kofi Boeteng ambaye ni mtaalamu wa kampeni za chanjo wa WHO amesema  japo wamepiga hatua kubwa katika kutoa  chanjo kutoka  asilimia 45 mwaka 2016 mpaka asilimia 56 mwaka jana  bado kuna changamoto kubwa kuwafikia  wananchi katika maeneo yalioko chini ya utawala wa wanamgambo ambao ni asilimia kubwa.

Mtaalamu  huyo pia anatilia mkazo suala la kuwapata wataalam uwa afya wenye uzoefu ili kuweza kutoa huduma bora na  yenye tija kwa wananchi ambao ndio walengwa wakubwa, na waliokwama katika sehemu mbalimbali isiyokuwa na huduma yenye kukidhi mahitaji  muhimu ya afya.  

WHO imesema  changamoto kubwa   wanalokabiliana nalo kutowafikia wananchi  walio wengi nchini Sudan kusini wakati wa kutoa chanjo ni pamoja na ushirikiano mdogo kutoka kwa vyongozi wa apande zote, miundombinu, ukosefu wa wataalamu na pia ukosefu wa takwimu sahihi za wananchi kutokana na hali ya usalama katika baadhi ya maeneo ambayo hayafikiki.