Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Brazili iwe mfano wa kuwaenzi wakimbizi:Grandi

kamishina mkuu UNHCR Filipo Grandi akihutubia mkutano wa  kimataifa kuhusu ulinzi wa wakimbizi nchini Brazil
Arthur Max/FM. Ministério das Relações Exteriores
kamishina mkuu UNHCR Filipo Grandi akihutubia mkutano wa kimataifa kuhusu ulinzi wa wakimbizi nchini Brazil

Brazili iwe mfano wa kuwaenzi wakimbizi:Grandi

Kamishina mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, Filipo Grandi amekutana na wawakilishi wa nchi 36 za Amerika ya kusini na  visiwa vya karibea nchini Brazil, katika mkutano wa kimataifa kuhusu ulinzi wa wakimbizi  ili kujadili  maswala nyeti yanayowababili wakimbizi katika ukanda huo.

Katika mkutano huo wa kimataifa, Grandi,  na  wawakilishi hao wamefikia  makakubaliano ya  kushirikiana katika kutoa hifadhi ya kudumu na pia kutetea  haki za watu wanaosaka hifadhi au kukimbia kachafuko nchini mwao ambapo amesema

Sauti ya Filipo Grandi

“Sinabudi kuishukuru serikali ya Brazil, kupitia waziri wa mambo ya nje kwa jitihada za kuandaa mkutano huu mihumu sana wa kikanda . Wakati umefika ambapo  ni lazma kusimamia misingi ya utu kama ilivyo desturi ya Amerika ya kusini na visiwa vya Karibea. Wakati huo huo tukikumbushia  ahadi ya Brazil katika kutoa kipaumbelekatika mkutano wa kimataifa kuhusu ulinzi wa wakimbizi.

Na kuhusu baadhi ya nchini za Amerika kusini na visiwa vya Karibea ambazo  bado zinaonyesha dalili za  kusuasua kufikia  mwakafaka katika makubaliano ya kimataifa kuhusu ulinzi wa wakimbizi na wasaka hifadhi mkuu huyo wa UNHCR amesema….

Sauti ya Filipo Grandi

Natumai nchi zingine za Amkerika kusini na visiswa vya Karibea pia zitatengeneza sera nzuri kuhusu ulinzi na hifadhi ya kudumu kwa wakimbizi kama ilivyo toa mfano   wa Brazil . Ushirikiano wa masuala ya uhamiaji baina ya baadhi ya visiwa vya Karibea na shirika la Umoja wa mataifa ya Uhamiaji IOM, ni hatua nzuri katika kukabili mapungufu yatokanao na sera mbaya ya uhamiaj katika baadhi ya nchi.