Jopo laundwa ili kutokomeza magonjwa yasiyoambukizwa: WHO
Afya
Shirika la afya duniani-WHO limetangaza kuundwa kwa jopo jipya la ngazi za juu ili kuweza kuchagiza hatua za kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukizwa NCDs, ambayo yameelezwa kuwa moja ya yaliyo mstari wa mbele kwa vifo vya binadamu. Magonjwa hayo ni kama vile saratani, ugonjwa wa moyo, mapafu na kisukari.