Hatua za wanawake India zashangaza wengi
Ajenda ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030 inatoa kipaumbele katika suala la ujasiriamali ikiwa ni njia mojawapo ya kutokomeza umasikini.
Umoja wa Mataifa na washirika wake wamekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu na pia fursa kwa asasi za kiraia, serikali mbalimbali duniani na pia mashirika binafsi ili kuimarisha ujasiriamali.
Wanawake nao kupitia mafunzo hayo hawajabaki nyuma bali wako mstari wa mbele kutumia fursa hizo za biashara katika kujiendeleza. Leo tunaelekea nchini India katika vijiji vya Bihar ambako wananawake 12 wamekuwa nguzo na pia mfano wa kuigwa, baada ya kuanzisha kampuni yenye mafanikio kwa msaada wa Benki ya dunia. Je wamefanya nini? Patrick Newman anafafanua katika makala ifuatayo.