Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Usugu wa viuavijasumu ni tishio duniani kote:WHO

Usugu wa viuavijasumu kusababisha dawa kukosa kutibu. Picha: WHO

Usugu wa viuavijasumu ni tishio duniani kote:WHO

Afya

Takwimu zilizotolewa leo na shirika la afya duniani WHO kuhusu usugu wa viuavijasumu au antibiotics zinaonyesha kwamba kiwango cha usugu wa dawa hizo dhidi ya maradhi kadhaa yanayosababishwa na bakteria au vimelea kiko juu katika nchi zote, za kipato cha juu , cha wastani na za kipato cha chini. Taarifa kamili na Assumpta Massoi

Takwimu zilizotolewa leo na shirika la afya duniani WHO kuhusu usugu wa viuavijasumu au antibiotics zinaonyesha kwamba kiwango cha usugu wa dawa hizo dhidi ya maradhi kadhaa yanayosababishwa na bakteria au vimelea kiko juu katika nchi zote, za kipato cha juu , cha wastani na za kipato cha chini. Taarifa kamili na Assumpta Massoi

(TAARIFA YA ASSUMPTA MASSOI)

Kwa mujibu wa mfumo mpya wa WHO wa ufuatiliaji wa kupambana na vijiumbe maradhi au antimicrobial ujulikanao kama (GLASS), takwimu hizo zimekusanywa kwa watu 500,000 walioathirika na vimelea na kutumia dawa kutoka nchi 22.

Ripoti inasema kuna takribani vimelea saba ambavyo ni sugu dhidi ya dawa za viuavijasumu vikiwemo Staphylococcus(STAFILOKOKAS) , E.coli (IKOLAI) na salmonella (SALIMONELA) ingawa ripoti hiyo haijajumuisha takwimu za vimelea vinavyosababisha ugonjwa wa kifua kikuu.

WHO inasema takwimu hizo zinathibitisha tatizo kubwa kote duniani. Hadi sasa kuna nchi 52 zilizoathirika na tatizo hili , 25 za kipato cha juu, 20 za kipato cha wastani na 7 za kipato cha chini ambazo zimeorodheshwa katika mfumo wa GLASS wa WHO. Dr Regina Mbindyo ni afisa wa WHO nchini Kenya anasema kwa upande wa Afrika na hasa Kenya

(SAUTI YA DR REGINA MBINDYO)

WHO imeongeza kuwa ripoti hii ni hatua ya kwanza muhimu kuelekea kuboresha uelewa kuhusu kiwango cha usugu wa viuajisasumu na kisha kuchukua hatua madhubuti dhidi ya tishio hilo kubwa la kimataifa.