Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watu milioni 25 kuchanjwa dhidi ya homa ya manjano Nigeria:WHO

Watu milioni 25 kuchanjwa dhidi ya homa ya manjano Nigeria:WHO

Afya

Shirika la Aflya ulimwenguni WHO kwa ushirikiano na serikali ya Nigeria, wamezindua kampeni kabambe  na kubwa kuwahi kufanyika ya chanjo dhidi ya  homa ya manjano kwa mwaka wa 2018 ikiwa na lengo la kuwafikia watu wapato milioni 25 kazikazini mwa Nigeria.

Shirika la Aflya ulimwenguni WHO kwa ushirikiano na serikali ya Nigeria, wamezindua kampeni kabambe  na kubwa kuwahi kufanyika ya chanjo dhidi ya  homa ya manjano kwa mwaka wa 2018 ikiwa na lengo la kuwafikia watu wapato milioni 25 kazikazini mwa Nigeria.

Kampeni hiyo iliozinduliwa  rasmi hii  leo ni  moja ya kampeni za kimataifa kusuhu chanjo ya homa ya manjano  kwa udhamini na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani UNICEF  pamoja na  GAVI unaolenga haswa majimbo ya kazikazini mwa Nigeria ya kogi, kwara na Zamfara, na baadae Borno.

Dr.Faisal Shwaib ambaye ni mkurugezi wa shirika la huduma ya afya nchini humo amesema kampeni hiyo ina lengo la kupunguza makali  na pia mambukizi ya homa ya manjano  nchini Nigeria  kwa asilimia 90 ikipakpo mwaka 2026.

Aidha amesema homa ya manajano ambayo huambukizwa kwa njia ya mbu , imeshamiri sana katika nchi za Afrika zilizoko kusini mwa jangwa la Sahara ambapo mwaka 2017, nchini Nigeria kumekuepo na visa 358 vya homa hiyo na kuwatu  45walipoteza maisha katika  majimbo 16.

WHO imekua msatari wa mbele katika kutoka  mafunzo kwa  wafanya kazi wa mashirika ya afya  ili kuweza kukabiliana na visa vinavyojitokeza kila siku  kuhusu vya homa ya manjano  nchini Nigeria na barani Afrika.