Mbio za Marathoni zaleta pamoja wakazi wa Goma na Kalemie
Katika kuadhimisha sikukuu ya krismas na mwaka mpya walinda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa huko Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, MONUSCO wameshiriki mbio za riadha za nusu marathoni kwenye mji wa Goma, jimbo la Kivu Kaskazini.
Mbio hizo ilikuwa ni sehemu ya kuhamasisha vijana na jamii kufanya mazoezi ambapo awamu ya kwanza ilihusisha walinda amani kukimbia kilometa 21 na awamu ya pili wananchi wapatao 250 walikimbia umbali wa kilometa 5.
Nako huko Kalemie ujumbe wa MUNUSCO uliandaa, michezo na burudani kwa watoto na kutoa zawadi kwa watoto wapatao 250 wenye umri wa kati ya miaka mitano hadi 17, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sikukuu ya krismasi.
Wakati wa sherehe hizo MONUSCO ilitoa dakika kadhaa kuwakumbuka walinda amani waliopoteza uhai wao katika kutimiza majukumu yao ya kulinda raia walio kwenye maaeneo ya mizozo DRC.