Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mbio za Marathoni zaleta pamoja wakazi wa Goma na Kalemie

Watoto huko Kalemie, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakiburudika kwa muziki wakati wa sherehe za krismasi zinazoendelea leo. Sherehe zimeandaliwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini DRC, MONUSCO. (Picha:MONUSCO)

Mbio za Marathoni zaleta pamoja wakazi wa Goma na Kalemie

Katika kuadhimisha sikukuu ya krismas na mwaka mpya walinda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa huko Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, MONUSCO wameshiriki mbio za riadha za nusu marathoni kwenye mji wa Goma, jimbo la Kivu Kaskazini.

image
Wafanyakazi wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakiwa katika mbio za nusu marathoni huko Goma. (Picha:MONUSCO)
Mbio hizo ilikuwa ni sehemu ya kuhamasisha vijana na jamii kufanya mazoezi ambapo awamu ya kwanza ilihusisha walinda amani kukimbia kilometa 21 na awamu ya pili wananchi wapatao  250 walikimbia umbali wa kilometa 5.

Nako huko Kalemie ujumbe wa  MUNUSCO  uliandaa, michezo na burudani kwa watoto na kutoa zawadi kwa watoto wapatao 250 wenye umri wa kati ya miaka mitano hadi 17, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sikukuu ya krismasi.

Wakati wa sherehe hizo MONUSCO ilitoa dakika kadhaa kuwakumbuka walinda amani waliopoteza uhai wao katika kutimiza majukumu yao ya kulinda raia walio kwenye maaeneo ya mizozo DRC.