Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ufugaji nyuki sasa ni mtaji dhidi ya umaskini huko Kyela, Tanzania

Utafiti mpya unaonyesha kuwa mashamba yasiyo na rutuba ya kutosha yanaweza kuongeza mazao kwa kuvutia wachavushaji wengi kwenye ardhi yao. Picha: FAO / James Cane

Ufugaji nyuki sasa ni mtaji dhidi ya umaskini huko Kyela, Tanzania

Kupitia lengo namba moja la kutokomeza umasikini lililomo kwenye ajenda ya  maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa  ya mwaka 2030, serikali zinahimizwa kutafuta mbinu mbadala kuwawezesha wananchi kupitia miradi mbalimbali ili kujikwamua na umasikini ifikikapo mwaka 2030.

Tanzania ni nchini mojawapo ambako serikali imechukua jukumu la kutoa elimu ya SDGs kwa kutafsiri malengo yao endelevu kwa lugha ya kiswahili ili kutoa mwongozo kwa wananchi na pili kuwapatia fursa za ujasiriamali kupitia miradi  mbalimbali kama  ufugaji, uvuvi, kilimo na kadhalika.

Lakini zaidi ya yote kuna ufugaji nyuki, ambapo Alex Punte wa redio  washirika ya Kyela FM kutoka Mbeya mkoani Tanzania amefuatilia ufugaji nyuki katika wilaya ya Kyela nchini Tanzania.