Buriani!
Leo imekuwa ni siku ya huzuni na majonzi makubwa nchini Tanzania ambako serikali, jeshi na wananchi na Umoja wa mataifa wamejumuika jijini Dar es salaam kuwaenzi na kuwapa mkono wa kwaheri mashujaa 14 walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka nchini humo waliouawa katika shambulio la wiki iliyopita nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC Assumpta Massoi na tarifa kamili
(TAARIFA YA ASSUMPTA MASSOI)
Natts…..
(SAUTI YA JEAN-PIERRE LACROIX )
"Nimekuja hapa kutoa rambirambi zetu kwa serikali , watu wa Tanzania na familia za walinda amani hao 14 kutoka Tanzania waliouawa na pia kutoa shukrani za dhati za Umoja wa Mataifa kwa Tanzania kwa uwajibikaji wao mkubwa katika masula ya amani na hususani ulinzi wa amani”
(SAUTI YA KASSIM MAJALIWA )
Akiunga mkono hoja hiyo kwa niaba ya Umoja wa Mataifa bwana Lacroix amesema
"Kutakuwa na uchunguzi wa nini kilichotokea , nini lkilichosababisha tukio hilo, bado ni mapema sana kufikia hitimisho lolote tunashirikiana na serikali ya Tanzania na nchi nyingine wachangiaji wa vikosi, ili kubaini nini hasa kimlichotokea na hatua gani tunaweza kuchukua pamoja ili kuwalinda vyema askari wetu na raia tunaowahudumia"
Kati ya wanajeshi hao 14 waliouawa baada ya kuvamiwa na kushambuliwa na kundi la waasi la ADF huko Kivu ya Kaskazini 12 wanatoka kisiwani Zanzina na wawili tanzania bara.