Ukimpa mwanamke fursa, jamii itanufaika
Kuna usemi wa kwamba ukimuelimisha mwanamke umeielimisha jamii na ukielimisha jamii basi utakua umeokoa kizazi cha baadaye. Huu usemi hauna maana ya upendeleo bali ni ukweli kwamba ukimpa mwanamke fursa basi jamii itanufaika zaidi. Hii inatokana na mapenzi, malezi, na moyo wa ujasiri aliojaliwa mwanamke.
Kwamaniki hiyo tunao mfano ya Bi Magdalena Namutebi mwanamke shupavu na shujaa, ambaye mbali na matatizo ya kufiwa na mume wake miongo mitatu iliyopita, peke yake alifanikwa kulea familia yenye zaidi ya watoto 9, kwa kuwapata fursa ya elimu na malezi bora. Tuungane na mwandishi weu John Kibego kutoka Uganda katika Makala hii.