Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utunzaji misitu ni jawabu la mabadiliko ya tabianchi

Washukiwa wakamatwa juu ya kuingilia na kuchafua hifadhi ya msitu ya serikali ya Bugoma. Picha: UM/John Kibego

Utunzaji misitu ni jawabu la mabadiliko ya tabianchi

Mkataba wa Paris kuhusu  mabadiliko ya tabianchi unaziasa serikali, mashirika ya kimataifa na asasi za kiraia duniani kote kuongeza jitihada  katika zoezi la kulinda mazingira.

Upandaji  miti na uhifadhi wa misitu miti ni moja ya hatua muhimu sana  katika kukabiliana na tatizo la ukame katika nchi nyingi kusini mwa jangwa la Sahara.

Nchini Uganda kampeni ya upandaji  miti na uhifadhi wa  misitu inaendelea vizuri kufuatia hatua ya serikali kuweka mkazo swala la ulinzi wa misitu. Mwandishi wetu John kibego alipata fursa ya kuwatembelea wananchi wa Rwangara nchini Uganda, ambao  wamekuwa wakihifadhi misitu kwa manufaa ya kulinda mazingira.