Miili ya walinda amani wa Tanzania waliouawa DRC yawasili Dar es salaam
Miili ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa 14 waliouawa katika mashambulizi huko kivu ya kaskazini, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongpo-DRC mwishoni mwa wiki iliyopita imewasili nchini Tanzania leo kwa ajili ya mipango ya mazishi. Lean Mushi na taarifa zaidi.
(Taarifa ya Leah Mushi)
Makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York nchini Marekani, bendera za nchi wanachama 193 hazijapandishwa katika milingoti hii leo na ya Umoja wa Mataifa ikipepea nusu mlingoti.
Hii ni ishara ya maombolezo ya walinda amani hao kutoka Tanzania waliouawa na wengine 53 kujeruhiwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Nimezungumza na Sylvia Mpanda dada wa mmoja wa marehemu Private Deogratius Kamili nikitaka kufahamu nini kinaaendelea kwenye ngazi ya familia
(Mahojiano)
Tayari Umoja wa Mataifa likiwemo Baraza la usalama la wamelaani vikali mauaji hayo na kusema kuwa yanafifisha juhudi za kutafuta suluhu katika jamuhuri ya kidemokrasia Kongo DRC.