Dola milioni 10.5 zitaokoa viumbe walio hatarini kutoweka :UNEP
Shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP, limepokea dola milioni 10.5 kutoka serikali ya Luxemburg, ikiwa ni mchango utakaosaidia kulinda aina za wanyamapori waishio mlimani ambao wako katika tisho la kutoweka.
Hahadi hiyoiliyotolewa leo kwenye mkutano wa mazingira mjini Nairobi Kenya, imekuja wakati UNEP inajiandaa na maadhimisho siku ya milima duniani hapo tarehe 11 mwezi huu. Shirika hilo limesema fedha hizo zitasaidia kulinda aina ya wanyama kama lengau, nyani na aina ya sokwe ambao tafiti zinaonyesha kua miaka 50 ijao kusipokuwepo na jitihada za kimazingira za kuwalinda, basi watatoweka katika uso wa dunia.
Bwana Erik Solheim mkurugenzi mtendaji wa UNEP, amesema kadri mabadiliko ya tabia nchi yanavyozidi kuenea ndivyo , aina za viumbe nyeti na pia maeneo ya asili yanavyoathirika. Hata hivyo amesema ufumbuzi wa mapema wa jinsi ya kukabiliana na tatizo la mazingira unaweza kusaidia kuhifadhi wanyamapori kupitia misaada kama iliotolewa na serikali ya Luxemburg.
UNEP imesema mpango mpya unaongozwa kwa ushirikiano na Luxemburg utazingatia kuboresha na kugawana maarifa na mbinu za ubunifu za mazingira ya kukabiliana na hali ya hewa.