Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahusika wa mauaji na ukatili dhidi ya Rohingya lazima wawajibishwe: Zeid

Raia jijini Rackhine, Myanmar. Picha: UNHCR

Wahusika wa mauaji na ukatili dhidi ya Rohingya lazima wawajibishwe: Zeid

Mkuu wa ofisi ya  haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa amelaani vitendo vya kikatili vya ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu  vilivyo pangwa na  kutekelezwa  dhidi  watu wa kabila la Rohingya, nchini Myanmar pamoja na miongo kadhaa ya ubaguzi na mateso kwa watu hao.

Bwana Zeid Ra'ad Al Hussein ameyasema hayo katika  kikao maalum cha baraza la haki za binadamu mjini Geneva Uswis wakati wa kujadili mustakabali wa watu wa kabila la  Rohingya walioko kaskazini mwa jimbo la Rakhine,kwa lengo la kuokoa maisha ya maelfu ya watu hao  dhidi ya  mauaji  ya kimbari yanaofannywa na vikosi vya serikali pamoja na wanamgambo.

Aidha Bwana Zeid amesema   katika ripoti ya watalaam huru wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa  kuhusu uchunguzi wa  vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu dhidi ya wati wa Rohingya mashahidi  ambao ni waatirika waliripoti vitendo vya udhalimu wa kutisha uliofanywa dhidi yao, ikiwa ni pamoja na kuchoma moto  kwa makusudi nyumba zao, mauaji ya kiolela dhidi yao na watoto wao na  pia ubakaji dhidi ya wanawake  .

Zeid ameongeza kuwa ulimwengu hauwezi kufumbia macho vitendo vya kikatili dhili ya waislamu wa kabila la Rohingya.  Lazima waliohusika wachukuliwe hatua za kisheria haraka iwezekanavyo.