Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatma ya uhamiaji wa kimataifa; Macho na masikio vyaelekezwa Mexico

Thomas Nguli mmakonde ambaye amepata uraia . Bwana Nguli na wenzake walihamia Kenya wakitokea Msumbiji. Kwa muda mrefu hawakuwa na uraia lakini hatimaye mwaka huu Kenya imewapatia uraia na wamakonde kutambuilwa kuwa ni kabila la 43 nchini Kenya. (Picha:UNHCR/Roger Arnold)

Hatma ya uhamiaji wa kimataifa; Macho na masikio vyaelekezwa Mexico

Mkutano wa kuandaa rasimu ya kwanza ya makubaliano ya kimataifa kuhusu uhamiaji unaanza leo huko Puerto Vallarta nchini Mexico, ikielezwa kuwa jambo la msingi ni kuhakikisha makubaliano hayo yanazingatia utofauti wa mahitaji ya wahamiaji kote ulimwenguni.

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhamiaji wa kimataifa Louise Arbour akizugumza na Idhaa hii amesema ujumbe wake kwa washiriki ni kwamba..

(Sauti ya Louise Arbour)

« Ujumbe ni kwamba iwapo tunataka kuzungumzia makubaliano ya kimataifa, ni lazima uwe wa kimataifa lakini uzingatia mahitaji tofauti ya kikanda. »

Mathalani amesema mahitaji ya wahamiaji barani Asia ni tofauti na mahitaji ya wahamiaji Afrika au barani Ulaya, hivyo amesema lazima serikali zitambue kuwa zinapaswa kutunga sera zinazokidhi mahitaji ya eneo husika.

Akizungumzia matarajio kutoka mkutano huo, Bi. Arbour amesema ni makubwa mno baada ya msururu wa vikao vya kikanda kujadili masuala yanayopaswa kuwepo kwenye makubaliano hayo kwa hivyo..

(Sauti ya Louse Arbour)

«Ni kutoka katika mkutano huu ambapo rasimu ya kwanza ya makubaliano hayo itatoka. Nchi wanachama zitaanza kuelewa maeneo ambayo wanakubaliana, wapi wanajikita zaidi, matumaini na matarajio. Tutakuwa pia katika nafasi nzuri baada ya

huu kuona wapi kazi inapaswa kufanywa zaidi, wapi kuna changamoto zaidi.”

Mchakato wa kikanda ulianza mwezi Aprili hadi Novemba mwaka huu.

image
Picha: Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhamiaji wa kimataifa Louise Arbour. UM/Ky Chung