Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WHO yatoa msaada wa vifaa vya tiba Libya

WHO yatoa msaada wa vifaa vya tiba Libya. Picha: UNSMIL

WHO yatoa msaada wa vifaa vya tiba Libya

Shirika la afya duniani  WHO limetoa msaada wa mitambo ya kusaidia kupumua kwa wangonjwa mahututi katika hospitali ya Tragen kusini mwa Libya

Msaada huo wa mitambo miwili pamoja na vipuri vyake vyote umetolewa kufuatia kuwepo na upungufu mkubwa wa vifaa hivyo vya tiba kwa wagonjwa mahututi na wenye kuhitaji usaidizi wa kupumua.

WHO imeeleza kujizatiti kuendelea kutoa msaada wa kibinadamu kwenye nyanja ya afya maeneo yote nchini Libya .

Fedha za kununulia vifaa tiba hivyo zimetoka kwenye mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa CERF