Guterres kushiriki mkutano wa AU-EU Abidjan
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric amezungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya umoja huo jijini New York, Marekani akiangazia masuala muhimu ya chombo hicho.
Miongoni mwao mambo hayo ni ziara ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa huko Abidjan nchini Côte d'Ivoire ambako anawasili leo tayari kuhutubia mkutano wa tano wa ushirikiano wa nchi za Muungano wa Afrika, AU na Muungano wa Ulaya, EU.
Maudhui ya mkutano huo ni kuwekeza kwa vijana kwa ajili ya mustakhbali bora.
(Sauti ya Stephane Dujarric)
“Wameripoti mashambulizi manne kwenye mji wa Kidal hii leo. Kambi tatu tofauti zilishambulia kwa makombora na roketi. Operesheni za msako zinaendelea. Ujumbe huo wa kulinda amani pia umeripoti kuwa leo asubuhi walinda amani waliokuwa kwenye doria walishambuliwa lakini hakuna aliyejeruhiwa. Tumekuwa tunalaani vitendo hivi ambavyo vinaweza kuwa uhalifu wa kivita kwa mujibu wa sheria za kimataifa.”