Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Takribani miaka 7 ya vita Syria, watu milioni 13 bado wanahitaji misaada- OCHA

Mhudumu wa afya wa UNICEF anapima mtoto kwa ajili ya kudhibiti utapiamlo nchini Syria. Picha: OCHA

Takribani miaka 7 ya vita Syria, watu milioni 13 bado wanahitaji misaada- OCHA

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA imetoa ripoti kuhusu madhara na uhitaji wa misaada ikiwa ni takribani miaka 7 tangu kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria.

OCHA inasema katika kipindi hicho, misaada  bado inahitajika sana  kwani  watu milioni 13.1, ikiwa ni wanawake, watoto na wanaume wanahitaji usaidizi wa kibinadamu.

Kati yao hao, milioni 5.6 wako kwenye maeneo hatarishi kuyafikia na wanahitaji msaada wa dharura  wa kuhamishwa kwa jili ya matibabu .

Aidha ripoti hiyo ya OCHA inaonyesha kuwa migogoro inayoendelea  huko Syria imekuwa chanzo kikubwa cha mahitaji ya kibinadamu, na idadi ya raia katika sehemu nyingi za nchi hiyo wanaishi kaitka hali hatarishi kwa maisha yao, hivyo kuaathiri  utu na ustawi wao kila siku.