Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM wachukizwa na ripoti za waafrika kuuzwa kama watumwa Libya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza na waandishi wa habari. Picha: UM

UM wachukizwa na ripoti za waafrika kuuzwa kama watumwa Libya

Kufuatia habari ya kwamba wahamiaji wa Afrika walioko nchini Libya wanauzwa kama watumwa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa na kueleza kushtushwa kwake na kitendo hicho.

(Sauti ya Guterres)

“Nimeshtushwa na habari na video vinavyoonyesha wahamiaji wa Afrika wakiripotiwa kuuzwa kama watumwa.”

Hivyo akasema..

(Sauti ya Guterres)

“Nachukizwa na vitendo hivi vya kusikitisha natoa wito kwa mamlaka zote zenye uwezo kuchunguza shughuli hizi kwa kina bila kuchelewa na kuwafikisha watekelezaji wa vitendo hivi mbele ya sheria.”

image
Idadi ya wahamiaji waliozuiliwa nchini Limbya katika hali mbaya yaongezeka. Picha: OHCHR
Bwana Guterres amesema tayari ameomba mamlaka husika kwenye Umoja wa Mataifa kuchukua hatua huku akisisitiza kuwa..

(Sauti ya Guterres)

“Utumwa hauna fursa katika dunia yetu. Na vitendo hivi ni miongoni mwa vitendo vya ukiukaji mkubwa wa  haki za binadamu na vinaweza kuwa uhalifu dhidi ya binadamu.”

Katibu Mkuu amesihi nchi zote kusaini na kuridhia mkataba wa kimataifa dhidi ya uhalifu unaovuka mipaka pamoja na itifaki zake huku akisihi nchi ziungane kupinga kitendo hicho na kuimarisha uhamiaji halali.