Neno la wiki: Bwela Suti
Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno "Bwela Suti". Mchambuzi wetu ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Nuhu anasema “Bwela Suti” ni "apron" au vazi analovaa mtu ili kuzuia uchafu wa mafuta ama vitu vyovyote vile kuharibu nguo zake, aghalabu au hususan hutumika jikoni, lakini pia linawezatumika katika mazingira mengine.