Tanzania tunaelekea kulinda amani CAR na Sudan Kusini- Dkt. Mwinyi
Mkutano wa masuala ya operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa umekunja huko Vancouver, Canada kwa lengo la kuangazia jinsi ya kuboresha operesheni hizo. Idadi kubwa ya operesheni ziko barani Afrika ambako mizozo na vita imegubika eneo hilo. Miongoni mwa washiriki alikuwa Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa kutoka Tanzania Dkt. Hussein Mwinyi. Kando mkutano huo Mathew Wells wa Idhaa ya Umoja wa Matafa alizungumza naye katika mahojiano haya ambayo maswali yataletwa kwako na Flora Nducha. Kwanza Dkt. Mwinyi anazungumzia Tanzania na oporesheni za ulinzi amani za Umoja wa Mataifa.