Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Serikali ya DRC yatakiwa kuheshimu haki na uhuru wa kukusanyika -Zeid

Picha / MUNUSCO/ Goma

Serikali ya DRC yatakiwa kuheshimu haki na uhuru wa kukusanyika -Zeid

kamishina mkuu wa  Haki za Binadamu  wa Umoja wa Mataifa  Zeid Ra'ad Al Hussein ametoa wito kwa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kusitisha vitisho na hofu dhidi ya watu wanaoandamana leo kote nchi na kuitaka serikali kuhakikisha usalama wa wananchi katika misingi ya haki za binadamu chini ya sheria za kimataifa.

Baada   ya serikali ya DRC kubadili tarehe ya uchaguzi  mwanzoni mwa mwezi huu na kutangaza sasa uchaguzi utafanyika Desemba 2018,  mashirika ya kiraia  na vyama vya upinzani waliandaa maandamano ya kitaifa kupinga maamuzi ya vikosi vya usalama  na  wakuu wa mikoa ya  Goma na Kinshasa ambapo yapiga marufuku mikusanyiko au maadamano yoyote nchini humo.

Hata hivyo kati ya tarehe 22 na 23 Oktoba, wanaharakati wa kisiasa  na wa upinzani 65 walikamatwa huko Lubumbashi, kusini Mashariki mwa nchi, suala ambalo ofisi ya haki za binadamu inaendelea kupiga vita na kuitaka serikali ya DRC kuheshimu haki za binadamu .

Bwana Zeid  ametoa wito kwa viongozi wa kisiasa  kuhakikisha wanaheshimu haki na uhuru wa kukusanyika,  ushirika wa amani na uhuru wa kujieleza na pi apande zote kutumia fursa hii kueneza amani kwa jamii yote nchini humo.