Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Programu ya uanagenzi ya ILO yaleta nuru kwa vijana Tanzania

Programu ya uanagenzi ya ILO yaleta nuru kwa vijana Tanzania

Shirika la Kazi Duniani ILO kwa kushirikiana na Serikali ya Norway wamesaidia vijana kwenye ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Afrika kuboresha stadi zao katika biashara na pia kuwapa fursa za ajira katika sekta mbalimbali kama vile za hoteli na utalii. Hii ni sehemu ya uanagenzi wa kuhakikisha wanafunzi wanapata mafunzo ya kinadharia na vitendo ili wanapomaliza masomo yao wawe na stadi za kutosha. Je wamefanya nini? Selina Jerobon amefuatilia makala hii.