Serikali ya Syria na Daesh walitumia silah za maangamizi-JIM Ripoti
[caption id="attachment_331311" align="aligncenter" width="625"]03hapanapalejimripoti
Kikosi kazi cha pamoja cha Umoja wa Mataifa na shirika la kupinga matumizi ya silaha za maangamizi OPCW kijulikanacho kama JIM leo kimewasilisha ripoti yake ya uchunguzi kuhusu matumizi ya silaha za kemikali nchini Syria kwenye kikao cha baraza la usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani na kusema pasi shaka silaha hizo zilitumiwa na pande zote katika mzozo , jeshi la serikali ya Syria na wanamgambo wa Daesh .
Bwana Edmund Mulet, ambaye ndiye mkuu wa JIM,akiwasilisha ripoti yake mbele ya baraza la usalama amesema wamefanya uchunguzi wa kina, wa kitaaluma na kisayansi katika mashambulizi ya kemikali Syria, ambapo zaidi ya watu 90 walipoteza maisha.
(MULLET CUT 1)
“Nimewasilisha hitimisho la matukio mawili tuliyochunguza mwaka huu ikiwa ni pamoja na matumizi ya silah za kemikali huko Khan Shaykhun April 4 mwaka huu na vikosi vya Jeshi la serikali ya Syria na matumizi mengine ya kemikali Septemba mwaka jana ambayoyalifanywa na wanamgambo wa Daesh Um Hosh.”
Aidha katika kufafanua mbinu zilizotumika kufikia hitimisho la uchunguzi huo amesema...
(MULLET CUT 2)
Tunashirikiana na watalaamu kutoka mashirika na taasisi mbalimbali, wanasayansi, wanajeshi na pia tunazihusisha mahabara huru katika kukusanya sampuli za kemikali na silaha zilizotumika katika maeneo tofauti na kuzifanyia uchunguzi wa kina ili kubaini ukweli.