Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mateso ya watoto vitani ni aibu yetu wenyewe- Guterres

Mateso ya watoto vitani ni aibu yetu wenyewe- Guterres

Kiashirio hicho cha kutoka kwa kiongozi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa mwezi huu wa Oktob, nafasi ambayo inashikiliwa na Ufaransa. Anatangaza kuanza kwa mjadala wa wazi  na hivyo kila mjumbe awe sawa.

Huyu ni Waziri wa Ufaransa anayehusika na masuala ya Ulaya na mambo ya nje Jean-Yves Le Drian na ameongoza mahsusi kikao hiki kinachoangazia watoto kwenye mizozo ya kivita.

Bwana Le Drian akampatia fursa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ili aweze kuhutubia wajumbe.

Nats-2-Guterres

Bwana Guterres anawaeleza wajumbe kuwa ripoti iliyo mbele yao kuhusu watoto katika mizozo kwa mwaka 2016 inaweka bayana kuwa watoto wameendelea kuathirika kwa njia mbali mbali kutokana na uamuzi na vitendo vya viongozi wa kisiasa na kijeshi.

image
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akihutubia Baraza la Usalama. Picha: UM/Rick Bajornas
(Sauti ya Guterres)

“Watoto duniani kote wanateseka na mizozo isiyokubalika. Hii ni chanzo cha aibu kubwa ya dunia. Kipindi husika kwenye ripoti kimeonyesha ukiukwaji mkubwa wa haki za watoto. Tunashuhudia vikundi vilivyojihami vikilazimisha wasichana na wavulaka kujilipua. Watoto wananyanyapaliwa kwa kutumimishwa na vikundi vilivyojihami. Watoto wanaswekwa rumande kwa uhalifu ambao hawajafanya. Na tunashuhudia pande kinzani kwenye mizozo wakizuia misaada ya kuokoa maisha ya watoto.”

Hivyo amesema,

(Sauti ya Guterres)

“Iwapo tutaacha kizazi kijacho kwenye kiwewe na kikiugulia machungu, tunakuwa tumewasaliti wale ambao tunawahudumia na tunajisaliti wenyewe.”

image
Mwakilishi wa Katibu Mkuu kwenye masuala ya watoto kwenye vita, Virginia Gamba akihutubia Baraza la Usalama. Picha: UM/Rick Bajornas
Mwakilishi wa Katibu Mkuu kwenye masuala ya watoto kwenye vita, Virginia Gamba akatumia fursa hiyo kuweka bayana kile walichoshuhudia..

(Sauti ya Virginia)

“Taarifa zetu za hivi karibuni zaidi zinaonyesha kuwa idadi ya watoto wanaotumikishwa na kutumika imesalia ni kubwa sana huko Sudan Kusini na Somalia. Mashambulizi dhidi ya shule na hospitali bado ni mengi mno huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.”

image
Watoto waliotumika jeshini nchini Sudan Kusini. Picha: UNICEF/2015/South Sudan/Sebastian Rich
Rais wa Baraza la Usalama Waziri La Drian akasoma taarifa ya rais iliyoridhiwa na wajumbe wote ambayo imetambua mapendekezo yaliyomo katika ripoti ya Katibu Mkuu kuhusu ulinzi wa watoto kwenye mizozo.

Mathalani wajumbe wamesema wameshawishika kuwa ulinzi wa watoto kwenye mizozo unapaswa kuwa jambo muhimu katika mkakati wa kimsingi wa kutatua mizozo na kuendeleza amani.

Baada ya kuhakikisha wajumbe wameridhia taarifa hiyo ya rais, ndipo Waziri La Drian akazungumza kwa niaba ya Ufaransa akisema kuwa

(Sauti ya La Drian)

“Tunatakiwa kusonga mbele na lengo letu la kuwa na dunia bila ya watoto kwenye maeneo ya vita. Tunapaswa kuwajibika kuhakikisha kuwa watoto wanakuwepo maeneo ambayo wanapaswa kuwepo. Mathalani shuleni na katika familia zao pendwa na badala ya kuwa kwenye maeneo ya vita. Huu ni wajibu wetu wa kimataifa.