Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ubunifu Burundi wahakikisha hedhi salama kwa wasichana

Ubunifu Burundi wahakikisha hedhi salama kwa wasichana

Idadi kubwa ya wasichana na wanawake nchini Burundi wana matatizo ya utumiaji  taulo za kike au sodo. Asilimia kubwa kutokana na ukosefu wa pesa wanatumia nguo, huku wengine wakitumia majani na hivyo kuwasababishia athari kubwa za kiafya . Shirika moja  la vijana nchini humo  la SACODE (SAKODE) baada ya kutafakari kero hiyo liliamua kutengeneza taulo za kike au sodo kwa vifaa vya nyumbani na kuipanga bei kuzingatia hali ya kipato cha wanawake nchini Burundi.Wasichana wengi  shuleni wamenufaika kwa kupewa taulo hizo za kike bila malipo. Mwandishi wetu wa Maziwa Makuu , Ramadhani KIBUGA  amefuatilia hali hiyo na ametuandalia makala  hii kutoka mjini Bujumbura, Burundi.