Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maisha ya mamilioni ya watoto hatarini ,majira ya baridi kali:UNICEF

Maisha ya mamilioni ya watoto hatarini ,majira ya baridi kali:UNICEF

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhumia watoto UNICEF, limetoa wito  wad ola milioni 60 kutoka kwa wahisani ili kusaidia kuokoa maisha yawatoto zaidi ya 1.5 katika majira yajayo ya baridi  kali na  theluji.

Mkurugenzi wa UNICEF  kanda ya Mashariki , Kati na Afrika Kaskazini, Bw Geert Cappelaere amesema pesa hizo zitasaidia kuokoa maisha ya watoto wengi walioko katika nchini zilizoathirika na migogoro ya kivita kama Iraq, Syria, Palestina na nchi jirani, na pia  watoto wanoishi  katika kambi za wakimbizi ukanda wa mashariki na mashariki ya kati.

Aidha Bw Geert amesma bila  msaada wa haraka, baridi inaweza kuwa pigo jingine kubwa kwa watoto walio katika mazingira magumu, akitolea mfano wa kupata magonjwa kama  mfano ya kifua  na  pumu .

Hivyo amesisitiza upatikanaji wa pesa uatasaidia katika ununuzi wa blanketi, nguo za kuongeza joto na mafuta ya petroli kwajili ya genereta za kupasha joto.